CHAMA CHA MAZINGIRA NA UFUGAJI TIJA TANZANIA (CHAMAUTA)

 “Tunza Mazingira, Fuga kwa Tija kwa Maendeleo ya Taifa”

MPYA Taarifa ya Usajili kidijitali MAELEKEZO YA NAMNA YA KUSAJILI WANACHAMA WAPYA MIKOANI:
Zoezi la Kusajili Wanachama wapya Kidigital huko Mikoani ni endelevu. Utaratibu ni kama ufuatao:-
1. Mwananchi aliye tayari kujiunga na CHAMAUTA anatakiwa kujaza Fomu ya kuomba kujiunga.
2. Kila Fomu ibandikwe Picha ya muombaji.
3. Fomu irudishwe makao makuu kwa njia ya mtandao (MAKAO MAKUU).
4. Fomu zikisha hakikiwa. Na malipo ya Kiingilio na Ada ya Mwanachama TShs. 10,000/- (elfu kumi tu) ikishawekwa kwenye namba Account ya CHAMAUTA, Benki ya CRDB.
5. KADI yake itatumwa mara moja kupitia Uongozi wa eneo husika (Wilaya au Mkoa). Hiyo ni njia moja. PILI Mahali wanapopatikana kwa wingi kwa wakati mmoja Wanachama wapya *300 - 500+.* Tutatuma Kikosi kazi cha Viongozi na Watalaam kwenda na vifaa kutoa na kukabidhi KADI papo hapo.

Pakua fomu hapa chini ya kujiunga CHAMAUTA kwa mtu binafsi.
Pakua fomu chini ya kujiunga  CHAMAUTA  kwa Kikundi/Taasisi/Kampuni.

KUHUSU SISI

Chama cha Mazingira na Ufugaji Tija Tanzania (CHAMAUTA) ni chama kilichoundwa na wadau mbalimbali wa utunzaji wa mazingira pamoja na ufugaji wenye tija hapa nchini. Wadau hao ni wale wanaofuga mifugo mbalimbali kama vile ng’ombe, kondoo, mbuzi, nguruwe, Samaki, Bata, Sungura n.k. Msukumo wa kuanzisha chama hiki unatokana na hitaji la kuongeza tija katika ufugaji na kutunza na kuendeleza mazingira ambayo mifugo hiyo hutegemea.

Chama kimesajiliwa kwa mujibu wa sheria ya usajili wa vyama vya Kijamii (The societies Act (CAP 337 R.E 2002) na Kupewa namba ya usajili S.A 23417 Ya tarehe 3 augost, 2023.

JEREMIAH JOHN WAMBURA
Mwenyekiti Taifa Chama Cha Mazingira na Ufugaji Tija Tanzania

Kazi ya Taasisi

 Kuunganisha Nguvu za wadau wote wa utunzaji wa mazigira na wafugaji wote Tanzania, ili kulinda na kutetea haki na maslahi yao kuimarisha na kutafuta Masoko ya mifugo na kuwajengea uwezo kibiashara na kiuchumi ili kuweza kujiendeleza. Kuhakikisha wafugaji wanapata maeneo bora ya malisho yenye kuendana na dhima nzima ya ufugaji wenye Tija na utunzaji wa mazingira

Taasisi inaamini katika Mambo yafuatayo

 Uwazi
Heshima
Uwajibikaji
Uzalendo
Kujitolea
Umoja
Kuzigatia Matokeo Chanya
Kazi kwa pamoja
Mazingira Rafiki
Ubora

Taarifa Mpya

Ajira

TANGAZO LA KUPATA WATAALAM/KAMPUNI WATAKAOSHIRIKI KATIKA MRADI WA SHAMBA LA NG’OMBE WA MAZIWA:  A. UTANGULIZICHAMAUTA ni Chama cha Mazingira na Ufugaji Tija Tanzania kilichoundwa nawadau mbalimbali wa utunzaji wa mazingira

Read More
Mazingira

Miradi

Miradi inayoanza kutekelezwa ni pamoja na Ufugaji wa kisasa wa Ng’ombe wa Maziwa na Kunenepesha. A) MIRADI YA UFUGAJI. CHAMAUTA tunatekeleza miradi Ifuatayo:a) Miradi ya ufugaji.b)Miradi ya Mazingira. 1.Mradi wa

Read More
Mazingira

Ziara

Mwenyekiti wa Chama Cha Mazingira Fuga kwa Tija Tanzania (CHAMAUTA) akiitambulisha Kamati Tendaji katika ofisi ya mkuu wa mkoa Dodoma.

Read More
Mazingira

Mkutano

Mwenyekiti wa Chama Cha Mazingira Fuga kwa Tija Tanzania (CHAMAUTA) akiwa na Waziri wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Mhe Abdallah Ulega

Read More

Leave a Reply